Jumanne, 29 Julai 2014

NEWS;#bum bum ya #diamond_platnumz inazidi kushika kasi ndani ya #TRACE URBAN

Ni ile video ya #bum bum iliyofanywa na hitmaker wa mdogomdogo @diamond_platnumz akimshirikisha msanii #iyanya kutoka nigeria na video yake iliofanywa na director mkubwa Africa @mr.moe_mussa.Sasa imeanza kushika kasi katika channel ile maarufu ya muziki Africa iitwayo#Trace_tv.Ni hatua nzuri sana kwa muziki wetu wa bongo na congratulation to u @diamond_platnumz fanya ufike mbali zaidi ya hapo

NEWS; Dully Sykes aelezea maana ya wimbo wake ‘Togola’

Dully Sykes ana wimbo mpya uitwayo Togola
uliotengenezwa katika studio zake za 4.12.
Akiongea na EFM hivi karibuni, Dully alidai kuwa
Togola ni salam ya kabila la kizigua.
“Togola maana yake kama salamu tu, kizigua
hicho,” alisema Dully. Unajua mwanaume
unapokuwa mwenyewe huna partner ndani ya
gari inabidi uanze kutizamatizama nikasema
‘mtizame’ lakini kutizamatizama unaweza
kumuona mmoja wapo nje ukashusha kioo
ukasema ‘hello, habari yako, salama’ hapo tayari
ushatogola. Na ndio maana inamaanisha hii
nyimbo kuwa ‘wewe bado ni kijana na unataka
msichana wa maana’, msichana wa maana ni yule
ambaye yupo tayari kuolewa.”

NEWS; Boko Haram wamteka mke wa makamu waziri mkuu wa Cameroon

Wanamgambo wa kundi la Boko Haram,
wamemteka mke wa makamu wa waziri mkuu wa
Cameron, na kuwaua watu watatu baada ya
kuushambulia mji wa kaskazini wa Kolofata.
Wanamgambo hao walivamia makazi ya waziri
Amadou Ali huko Kolofata na kumteka mke wake.
Kiongozi wa dini ambaye pia ni meya wa mji huo
Seini Boukar Lamine naye alitekwa katika
shambulio tofauti.
Boko Haram, kundi la wanamgambo wa kiislamu
la Nigeria limeingia Cameroon hivi karibuni
baada ya nchi hiyo kutuma wanajeshi kuungana
na majeshi ya kimataifa kupambana na
wanamgambo hao.

PICHA; Wema Sepetu aivaa jezi ya Michael Jordan (23), asherehekea Eid na shemejiye, Dimpoz

Wema Sepetu ni shabiki wa mchezaji wa zamani
wa kikapu wa timu ya Chicago Bulls, Michael
Jordan?
Mapenzi yake kwa mchezaji kikapu huyo tajiri,
yameonekana kwenye picha alizopiga wiki hii
(kama sio Jumanne hii) akiwa amevaa jezi
nyeupe ya Chicago Bulls yenye namba 23, namba
aliyokuwa akitumia Jordan. Jezi hiyo imempenza
zaidi Mrs Naseeb baada ya kuisindikiza na tight
yekundu na chini akipigilia sneakers kali.
Wema alikuwa akispend sikukuu ya Eid na
shemeji yake, Ommy Dimpoz aliyekuwa amevaa
kanzu.

NEWS;alichosema #dudubaya kuhusu bifu la allykiba na diamond

Dudubaya anajulikana kama mmoja wa Wasanii
wa siku nyingi bongoflevani ambae pamoja na
headlines zake binafsi huwa anasikika mara
chache akizungumzia au kutoa ushauri kwa ishu
kadhaa za Wasanii wenzake.
Baada ya kusikia yanayoendelea kati ya mastaa
wa bongofleva Diamond na Ally Kiba kwamba
wako kwenye beef, Dudubaya alikutana na
Mimi blogger Dar es salaam na kuyasema yafuatayo >>
‘Wasanii wa Tanzania tuna wapambe na sio
marafiki kwa sababu mpambe unaweza kuwa
umelewa yeye ndio anakoleza ugomvi lakini
rafiki ni yule anaekuonya au kukushauri’
‘Ali Kiba alifanya ngoma na R.Kelly nikafurahia
na nikapenda kinoma kupiga salute kwa mdogo
wangu anakwenda next level, Diamond kaja
kufanya vizuri na ninafurahia… muziki huu
unakosa nguvu kwa sababu ya roho mbaya, wivu
na chuki na kutokuwa makini na
wanaotuzunguka, anakwenda kwa Diamond
anasema hivi kisha anakwenda kwa Ally Kiba
anasema hivi’ – Dudubaya
‘Ninachowashauri hawa wadogo zangu watulie
chini wajitambue ni Wasanii na usanii wao ni
wa kutengeneza pesa, tena watengeneze hata
Tour ya Amani wazunguke nchi nzima..
wazunguke hata Afrika Mashariki na sio hizi
beef’
‘Siku moja nilikua na Dully Sykes na Christian
Bella alafu watu wakawa wanasema Diamond
ooohhh sijui kashindaje tuzo saba, nikawaambia
hivi ukiwa na akili timamu wimbo kama ‘my
number one’ kila kona unayopita, video mpaka
TV za kimataifa zinapiga alafu leo unaweza
video yako ya kijingajinga unategemea
kuishinda ‘my number one’ …….Diamond
alistahili kushinda hizo tuzo saba, mimi sikuona
cha ajabu’
Kwenye sentensi nyingine Dudubaya amesema
‘kuna gazeti moja liliandika eti Diamond
alihonga hela kuchukua hizo tuzo, ni vitu vya
kipumbavu kabisa… hujui kusoma lakini picha
lazima uione, Ali Kiba na Diamond kila mmoja
ana mama yake, wakae chini kama binadamu
wajitambue, waachane na mambo ya watoto wa
hapa mjini hawa ni wapambe tu mwisho wa
siku hawana msaada’

NEWS; Kuhusu simu ya ajabu aliyopokea Tunda Man July 28

Kuna kipindi stori za namba ambazo wengi
walikua wakisema za ajabu na endapo
zikikupigia usipokee zilikuwa zikitawala sana
kwenye mitandao ya kijamii na wengi pia
walikua wakizonyesha namba hizo.
Tunda Man ambaye pia ni miongoni mwa watu
wanaounda kundi la Tip Top Connection Jioni ya
July 28 amepata simu hiyo ambayo amedai
kwake ilikua ni mara ya kwanza kupigiwa kwani
namba hizo hajawahi kuziona zikimpigia kabla

Tunda man ameongea na mimi na
kusema>>’Nilikua nafuturu jana jioni wakati
naendelea kufuturu nikapigiwa simu namba
sikua nazijua kwani zilikua za maajabu
tu,sikupokea,ilipiga kama mara 30 hivi’
‘Baadae nikapokea na kisha nikaiweka mbali
kidogo na mimi wakati nasema hallow ghafla
kitu kama shoti ya umeme kikaanza kutembea
kwenye viganja mpaka kwenye mkono nikakosa
nguvu kabisa nikawaambia jamani nipelekeni
hospital’
‘Tukaenda hospital ya Serikali hapo
Palestina,Dokta akasema huu ugonjwa tangu
ameanza kutibia watu hajakutana nao ni mara
yake ya kwanza hivyo matibabu aliyokuwa
akinipatia ni kama ya mtu aliyepooza ghafla’
‘Kwa sasa namshukuru Mungu naendelea vizuri
ingawa kuna dawa nimepewa zingine nameza
mara 2 kwa siku na vidonge vingine ni mara 3
kwa siku pia nimechomwa sindano’
Hii ndiyo namba iliyompigia Tunda

NEWS: Ushahidi mpya wa Chris Brown kuwa bado ana mapenzi kwa Rihanna

Kila mtu ana story yake ya uhusiano wake na
mpenzi wake lakini hii story ya Chris Brown na
Rihanna inachukua attention ya watu wengi
kutokana na mambo yanayoendelea kati yao.
Kila muda ukipita inatokea tetesi kwamba Chris
Brown ana mawasiliano ya siri na Rihanna lakini
bado hakukuwa na ushahidi kuthibitisha hilo.
Kitu kipya hivi sasa kinachotafsiriwa kwamba
bado Chris ana mawazo na kumbukumbu juu ya
uhusiano wake na Rihanna ni kutokana na
picha ya rafiki wa Rihanna. Melissa Ford ambaye
ni rafiki wa karibu wa Rihanna ali post picha ya
Chris na Rihanna na kuandika kuwa ni hao ndio
couples anaowapenda.
Baada ya hapo Chris Brown ali like hiyo picha
na kuonyesha kwamba amefurahia hiyo post.
Kutokana na ukaribu wa Rihanna na Melissa sio
rahisi kwa Melisa ku post picha hiyo kama
mambo bado ni mabaya kati ya Riri na Chris.
Kama kuna lolote linaendelea kati ya Chris
Brown na Rihanna lazima Melissa Ford awe
anajua kwasababu wapo karibu sana.
Wachambuzi wanasema kwamba kuna kitu
kinaendelea chini kwa chini kati ya Chris Brown
na Rihanna na hivi karibuni kinaweza kuwekwa
wazi.

NEWS: Shakira ni mjamzito tena? Hiki alichokisema Gerard Pique

Kwa mara nyingine tena familia ya mwanamuziki
maarufu duniani Shakira na mchumba wake
mwanasoka, Gerard Pique  - imeingia kwenye
‘headlines’ za vyombo vya haari ulimwenguni.
Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ukiwemo
mtandao wa tracetv unaripoti kwamba
mchumba wa Shakira, Gerard Pique amekaririwa
akisema hitmaker wa ‘Hips Dont Lie’ ni
mjamzito kwa mara nyingine tena.
Kulikuwepo na tetesi nyingi hasa baada ya
Shakira kutumbuiza kwenye kombe la dunia
liloisha hivi karibuni nchini Brazil, lakini kambi
ya Shakira ilikanusha uvumi huo.
Lakini jana kupitia channel ya kilatino ya “Fox
News” – kituo hicho cha TV kiliripoti kwamba
Pique amewathibishia kwamba Shakira ni
mjamzito.
Pique na Shakira tayari wana mtoto mmoja wa
kiume waliyempa jina la Milan, ambaye alizaliwa
mnamo mwaka 2012, miaka miwili baada ya
wazazi wake kuanza mahusiano yao wakati wa
utengenezwaji wa wimbo wa kombe la dunia
2010.

NEWS:Nicki Minaj anamiliki headlines kwenye internet na hizi picha

Ikifika tarehe tarehe 4 mwezi wa 8 mashabiki
wote wa Nicki Minaj watafungua iTunes
kununua wimbo mpya wa Nick Minaj unaitwa
Anaconda. Lakini hivi sasa kick kubwa ni cover
ya picha za wimbo huo ambayo alipost kwenye
instagram na hadi hivi sasa imepata likes zaidi
ya milioni 3.
Picha ya kwanza imepigwa kutoka kwa nyuma na
hivi sasa ametoa nyingine iliyopigwa kutoka
mbele.

Jumapili, 27 Julai 2014

POST ZA MASTAA WETU WA BONGO #INSTAGRAM

Screen Shot 2014-07-26 at 4.03.18 AMInstagram ni mtandao mwingine wa kijamii unaozidi kupata Wanachama wapya kila siku kutokana na aina yake ya kupost pichaz ambapo umekua ukitumiwa sana hata na watu maarufu na kurahisisha kazi ya kusambaza habari kama unavyoona baadhi ya mastaa kwenye hii post.
Screen Shot 2014-07-26 at 3.02.48 AM
Hii ni caption ya Diamond kwenye hiyo picha hapo juu akiwa Dallas nchini Marekani kuhudhuria tuzo za Afrimma.
                                                                                                ******************************
Screen Shot 2014-07-26 at 3.00.41 AMMJ Records imepata studio mpya? amepost hii picha C.E.O mwenyewe Master J na kuandika haya maneno hapa chini…
Screen Shot 2014-07-26 at 3.06.46 AM                                                                                                ******************************
Screen Shot 2014-07-26 at 3.09.57 AMMwigizaji Kajala baada ya kuweka hii picha akaandika ‘Mtu anapokwambia huwezi kufanya kitu flani usiache kukifanya, tabasamu na kusema nitakuonyesha’
Screen Shot 2014-07-26 at 3.12.40 AM

                                                                                ******************************
Staa wa bongoflevani Nay wa Mitego yuko nchini Kenya kufanya video yake mpya ambayo ameshea moja ya picha ya utengenezwaji wake kama unavyoona hapa chini…
Screen Shot 2014-07-26 at 3.18.27 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.18.36 AM
                                                                                 ******************************
Saa kadhaa baada ya kusambaza single zake mbili mpya kwenye Radio Stations mbalimbali Tanzania, mwimbaji Ali Kiba amepost hii kwenye instagram na kuambatanisha na hiyo caption chini yake.
Screen Shot 2014-07-26 at 3.26.52 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.26.59 AM
                                                                                        ******************************
Ifuatayo ni TBT ya CMB Prezzo kutoka Kenya.
Screen Shot 2014-07-26 at 3.25.09 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.25.40 AM
                                                                              ******************************
Jokate yuko nchini Kenya ambako kwa July 25 pekee ameonekana akihojiwa kwenye vyombo viwili vya habari kama alivyopost hapa chini akiwa na Mtangazaji William Tuva wa Citizen TV/Radio.
Screen Shot 2014-07-26 at 3.40.03 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.40.11 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.36.38 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.36.54 AM
                                                                                  ******************************
Hapa chini ni meneja wa kundi la Tiptop Connection ambae pia ni meneja wa Diamond Platnumz Babu Tale ambae ameshafika Marekani na Diamond kuhudhuria tuzo za AFRIMMA.
Screen Shot 2014-07-26 at 3.28.06 AM
Screen Shot 2014-07-26 at 3.28.23 AM                                                                            ******************************
Ni halali yako kupata kila kinachonifikia mtu wangu na niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>> twitter Insta FB

#NEWS: Mtangazaji wa 102.5 Choice FM kuiwakilisha Tanzania kwenye kongamano la Obama

U.S. Embassy Public Affairs Officer Ms. Marissa Maurer kushoto akikabithi ticket kwa Mtangazaji kutoka Clouds Media group (Choice FM 102.5)  Louissa Babbie Kabae ambae pia ni brand Manager kushiriki kwenye U.S. Commitment to Africa Reporting Tour kuanzia July 26 through August 8 nchini Marekani.
Kabae ataungana na Waandishi wengine zaidi ya 20 kutoka nchi mbalimbali Afrika kwenye tour Washington DC na kwenye jiji la Atlanta kwa ajili ya U.S – African Leaders Summit and Young African Leadership Initiative (YALI) Forum hosted by President Obama.
These two initiatives build on, and seek to further strengthen partnership between United States and Sub-Saharan Africa  in strengthening democratic institutions, accelerating economic growth,  promoting trade and investments, advancing peace and security and investing in the next generation of African leaders. For more information about the events visit.Screen Shot 2014-07-26 at 5.46.05 AM

WAIMBAJI WA INJILI AKIWEMO #BAHATI BUKUKU WAPATA AJALI

Gari lenye namba IT 7945 Toyota Nadia likiendeshwa na EDSON MWAKABUNGU (31) mkazi wa Tabata Dar es Salaam liliacha njia na kugonga gema na kusababisha majeraha kwa watu watatu baada ya kugongwa na gari jingine linalosadikiwa kuwa Fuso.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi David  Misime SACP amesema ajali hiyo imetokea tarehe 26.07.2014 saa tisa alfajiri katika barabara kuu ya Morogoro – Dodoma eneo la Ranch ya NARCO Wilaya ya Kongwa.
Waliojeruhiwa ni EDSON MWAKABUNGU ambae analalamika maumivu sehemu za vidole vya miguu yote, BAHATI BUKUKU (40) ambae ni mwimbaji wa nyimbo za injili na mkazi wa Tabata – Dar es Salaam ambaye analalamika maumivu sehemu mbalimbali za mwili wake.
Mwingine ni FRANK CHRISTOPHER (20) mwimbaji pia wa nyimbo za injili mkazi wa Tabata Dar es Salaam ambapo kapata michubuko usoni na mkono wa kulia.
Wote wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kongwa kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri ambapo Kamanda Misime amesema walikuwa wanatokea Dar es Salaam ambapo dereva alikuwa anelekea DRC – Kongo, BAHATI d/o BUKUKU na FRANK s/o CHRISTOPHER walikuwa wanakwenda Kahama kwenye tamasha la Injili.
 Uchunguzi wa ajali hii unaendelea ikiwa ni pamoja na kutafuta gari lililowagonga.

MATOKEO YA TUZO ZA #AFRIMMA 2014 AMBAZO #DIAMOND.. ALIKUWA AKIWANIA




Zinaitwa African Muzik Magazine Awards ambapo za mwaka huu 2014 zimetolewa huko Eisemann center Texas Marekani na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali akiwemo Diamond wa Tanzania ambae pia alikua mmoja wa wanaowania tuzo.
Good news za ushindi wote huu ni kwa mujibu wa meneja Babu Tale ambae nae kahudhuria tuzo hizi Marekani alienitumia msg kwa kusema wametangaza ukumbini kwamba Diamond ameshinda tuzo mbili moja ya Msanii bora wa Afrika Mashariki na nyingine ni wimbo bora wa kushirikiana ambao ni ‘number one rmx’ alioufanya na Davido wa Nigeria.


http://i0.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/07/Screen-Shot-2014-07-27-at-9.43.50-AM.png
Kolabo bora ni tuzo iliyokua inawaniwa na single ya T Pain na 2 Face – rainbow, Khona ya Uhuru na Mafikizolo wa South Africa, Surulere remix ya Dr Sid wa Nigeria, Mkenya Amani ft. Waganda Radio na Weasel ‘kiboko changu’ J Martins ft. Dj Arafat ‘touching body’ na Rebees na Wizkid ‘slow down’
Tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika Mashariki aliyoishinda Diamond ilikua inawaniwa pia na Ben Pol kutoka Tanzania, Bebe Cool wa Uganda, Wyre wa Kenya, Navio wa Uganda na Jackie Gosee wa Ethiopia.
Screen Shot 2014-07-27 at 8.17.01 AMLady Jaydee ameshinda tuzo ya Msanii bora wa kike Afrika Mashariki aliyokua anashindania na Rema wa Uganda, Aster Aweke wa Ethiopia, Avril wa Kenya, Victoria Kimani wa Kenya na Irene Ntale wa Uganda.
Producer bora wa mwaka ni Mtanzania Sheddy Clever aliekua anashindana Dj Oskido wa South Africa, Don Jazzy wa Nigeria, Shizz wa Nigeria, Killbeatz wa Ghana, Oskido wa South Africa, Nash Wonder wa Uganda na Ogopa wa Kenya.
Tuzo ya Mtayarishaji bora wa video imekwenda kwa Ogopa Dj’s ambao ndio waliifanya ile video ya kwanza ya ‘My number 1′ ya Diamond Platnumz.
Screen Shot 2014-07-27 at 8.17.33 AM
Tuzo zenyewe zimetolewa kwenye hili jengo
Stori zaidi na pichaz vitafata baadae hivyo endelea kukaa karibu na millardayo.com mtu wangu ili ujue kilichotokea kwenye tukio hili ambalo limewahusisha wakali wengine kama Davido, 2Face, Fally Ipupa, Iyanya, Flavour, Wyre, Miriam Chemmoss na wengine ambao ni sehemu ya watu kutoka nchi 17 za Afrika.
Ni halali yako kupata kila kinachonifikia mtu wangu na niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa